Trakti

Hofu ni nini? Hofu ya Mungu Hofu ya wakati ujao Hofu ya kushindwa Hofu ya mateso Hofu ya kifo Hofu, adui wa siri, huvamia watu wa kila umri na utaifa, na kila hatua ya maisha. Ni hila na ya kuumiza, hutia sumu namna yetu ya kufikiri, huiba furaha yetu ya ndani, na huua hamu yetu ya kuishi. Inatufanya tuwe na wasiwasi, wanyonge, wenye mshituko, wenye mahangaiko, kukasirika na wenye moyo dhaifu: Ni hisia gani hizi mbaya sizizohitajika!

Amani 7 minutes

Maisha ni magumu. Mateso na magumu ni sehemu ya maisha yetu. Watu wengi kwa wakati mwingine wanaugulia magonjwa ya kimwili. Njaa inawashikia watu kwa asilimia kubwa hapa duniani. Umasikini unawatesa watu wasio na uwezo. Na wengine wapo wanaoteseka mikononi mwa watu kwa namna mbalimbali. Kwa mfano, baadhi wanashikwa na matatizo ya kindoa, au wazazi wakatili, au mabwana wakali. Kwa sababu ya hali ya vita katika baadhi ya nchi zingine watu wengi wasio na hatia wanapoteza mali, nyumba, familia, na hata maisha yao. Wale wanaomtumikia Mungu kwa uaminifu, wanateswa na kuudhiwa kwa sababu ya imani yao. Ulimwenguni pote watu mamilioni wanateseka kila siku. Kwa nini?

Amani 6 minutes

Biblia hutuambia kwamba Mungu anajua kila kitu, na kwamba anahifadhi maandishi ya kumbukumbu za maisha yetu. Tutahitajika kutoa maelezo ya aliyoandika siku ya hukumu (Warumi 14:11-12). “Na niliwaona wafu, wadogo kwa wakubwa wamesimama mbele ya Mungu; na vitabu vilifunguliwa: na kitabu kingine cha uzima kikafunguliwa, na wafu walihukumiwa kwa yale yaliyoandikwa katika vitabu kulingana na kazi zao” (Ufunuo 20:12). Tutakaposimama katika hukumu mbele ya Mungu, tutakuwa tumechelewa kubadilisha maisha yetu wala mwisho wetu wa milele.

Wokovu 4 minutes

Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na nchi. Aliumba jua, mwezi, na nyota, na pia mimea na wanyama. Siku ya sita, aliumba mtu kwa mfano wake na akampulizia puani pumzi ya uhai. Mtu huyu wa kwanza alikuwa Adamu, na jina la mkewe aliitwa Eva. Mungu aliwapa makao ya kuishi katika bustani nzuri ya Edeni. Mungu aliwapenda Adamu na Eva, nao walimpenda Mungu. Mungu alimwagiza Adamu kuitunza bustani. Mungu aliwaambia kua wanaweza kula chochote watakacho isipokuwa kwa mti wa ujuzi wa mema na mabaya, na ya kuwa watakufa kama hawatatii.

Baadaye, Injili, Mbinguni, Color 3 minutes

Imeandikwa na John Reynolds Mojawapo ya mifano iliyohai na ya kuvutia kabisa ya kurudishiwa uhai wa mtu aliyekwisha kufa ambao nimewahi kuufahamu ulikuwa ni ule wa George Lennox, mwizi stadi wa farasi kutoka Jimbo la Jefferson (Marekani). Alikuwa akitumikia kifungo chake cha pili. Jimbo la Sedwick lilimpeleka gerezani kwa mara ya kwanza kwa kosa hilo hilo – wizi wa farasi.

Baadaye 11 minutes
Wokovu 13 minutes

Je, wewe ni mwenye furaha? Au hofu na hatia huondoa furaha yako yote? Je, ungetamani kuondoa hatia yako, lakini hujui kwa njia gani? Huenda unajiuliza, “Je, nitawahi kuwa mwenye furaha tena?” Ninayo habari njema kwa ajili yako. Kuna Mmoja awezaye kukusaidia, kusamehe dhambi zako, na kukupa furaha ya daima. Jina lake ni Yesu. Ngoja nikuambie habari zake. Mungu ndiye mwenyewe aliyeumba ulimwengu na vitu vyote vilivyomo. Alikuumba wewe na mimi.

Yesu 3 minutes

Lengo la Biblia Takatifu silo kuangalia hasa Shetani na kazi zake. Japokuwa tunapata mengi kwenye Biblia yanayofunua tabia zake na kazi zake. Wakati fulani Shetani alikuwa malaika, lakini aligeuka kinyume cha Mungu, Muumba wake, na akatamani kuwa kama Mungu. Matendo ya ufalme wa giza wa Shetani siyo mageni. Yanaonyesha dhahiri jitihada za Shetani kwa miaka kupingana na Ufalme wa Mungu. Anatoa mbadala wa kile ambacho Mungu anatimiliza kwa kupitia nguvu za Roho Mtakatifu.

Wokovu 6 minutes

Je, ni kwa “njia ya Yesu Kristo”? Au ni kwa “njia ya kimwili”? Njia ya Yesu Kristo ni njia nyembamba. Inaongoza kwenda Mbinguni. Huko Mbinguni hakutakuwa na huzuni wala maumivu, bali furaha na faraja pamoja na Yesu na malaika watakatifu. Njia ya kimwili ni njia pana. Inatuelekeza kwenye maangamizi, yaani Jehanamu, mahali ambapo kutakuwa na maumivu, maombolezo, na kusaga meno. Ili kuenenda katika njia ya Yesu Kristo, lazima tuachane na njia ya kimwili. Yesu alisema, “Mtu yeyote akitaka kuwa mfuasi wangu, lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.” (Mathayo 16:24). Je, kujikana nafsi kunamaanisha nini?

Cultural, Africa 4 minutes